Magazeti leo Februari 12,2026

BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) limewataka viongozi wapya wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) kuwa wabunifu ili kukuza vipaji vya vijana na kurejesha heshima ya mchezo huo nchini.
Akizungumza Februari 11, 2026, katika hafla ya makabidhiano ya vifaa iliyofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, Afisa Michezo wa BMT, Apansia Lema, amesema viongozi hao wana jukumu la kuinua kiwango cha netiboli kwa kuhamasisha ushiriki wa wasichana na kuibua vipaji mikoani kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania kimataifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa CHANETA, Stella Mwangomale ameahidi kushirikiana na viongozi wenzake kuimarisha mchezo huo huku aliyekuwa mwenyekiti, Dk. Devotha Marwa akiwataka kuendeleza mafanikio yaliyopatikana ili netiboli iendelee kuitangaza Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here