Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka wananchi wa Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kushiriki kikamilifu katika kuibua, kujenga na kuendeleza miradi ya maendeleo katika kata zao ili kuharakisha maendeleo ya jamii na kutimiza Dira ya Taifa ya kujenga uchumi imara na ustawi wa wananchi.


Akizungumza katika nyakati tofauti tarehe 11 Julai, 2026 wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo katika Kata ya Masasi, Mhe. Mahundi amesema maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana kwa Serikali pekee bali yanahitaji ushiriki wa wananchi, sekta binafsi na wadau mbalimbali wenye moyo wa kuchangia maendeleo ya maeneo yao.“Wananchi wanapaswa kuendelea kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kuwa ndiyo msingi wa kuboresha huduma za kijamii na kuinua ustawi wa jamii. Ushirikiano huu unasaidia kuijenga Tanzania yenye maendeleo endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho” amesema Naibu Waziri Mahundi.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo












