Magazeti leo Februari 16,2026

MAKUMBUSHO ya Taifa imetangaza shindano la kizalendo la kuimba wimbo wa Taifa “Tanzania Tanzania”, linalolenga kuhamasisha uzalendo, kudumisha utambulisho wa Taifa, na kuitangaza Makumbusho ya Taifa, ambapo mshindi wa shindano hilo atajipatia zawadi ya Shilingi 5,000,000.
Shindano hilo limeandaliwa kutokana na changamoto ya ukosefu wa uelewa wa jamii kuhusu Makumbusho ya Taifa na malengo yake. Shindano hilo linafungua fursa kwa mtu yeyote mwenye sauti ya kuvutia, hususan wanamuziki wenye ujuzi, kushiriki kwa kuongeza ubunifu na hisia katika kuimba wimbo huo.

Washiriki wanatakiwa kufuata taratibu maalum katika kuwasilisha wimbo wao. Miongoni mwa masharti ni kuandaa video itakayokuwa na utambulisho wa mshiriki na kutaja watu wa tatu, mshiriki anatakiwa kuvaa vazi la kizalendo lenye rangi za bendera ya Tanzania au vazi lolote la asili litakaloakisi utamaduni wa Tanzania, kama vile kitenge au batiki.

Vigezo vingine vya kushiriki ni kurekodi sauti na video zenye ubora wa hali ya juu zisizozidi dakika mbili. Washiriki pia wanashauriwa kutumia hashtags maalum zitakazorahisisha ufuatiliaji wa wimbo wao, zikiwemo: #Tumerithishwa #Tuwarithishe #UrithiWetu #FahariYetu #MuseumsTZ #KaziNaUtuTunasongaMbele.

Shindano hili lililoanza Februari 10 hadi Machi 20, 2026 linatarajiwa kuongeza uelewa wa Watanzania kuhusu historia, utamaduni, na umuhimu wa Makumbusho ya Taifa, huku likiwahamasisha kuwa mabalozi wa uzalendo kupitia muziki.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here