Magazeti leo Julai 7,2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe linamshikilia Juhud Mkosa (30), mkazi wa Kijiji cha Kijombe, Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe, kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi baada ya kumshutumu kuhusika na ushirikina uliodaiwa kusababisha mimba za mke wake kuharibika mara kwa mara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Mahamouda Banga, amesema uchunguzi wa awali unaonyesha mtuhumiwa alitekeleza mauaji hayo Novemba 29, 2025, dhidi ya baba yake, Ernesto Mkosa. Amesema baada ya mahojiano, mtuhumiwa alikiri kutenda tukio hilo.

Akizungumzia sababu ya tukio hilo, Kamanda Banga amesema mtuhumiwa alidai kuwa baba yake ndiye aliyekuwa akihusika na kuharibika kwa ujauzito wa mke wake kupitia vitendo vya ushirikina.

"Sababu halisi iliyopelekea mtuhumiwa huyu kutekeleza mauaji hayo ni kumtuhumu mzazi wake kwa ushirikina, akidai mke wake alikuwa akibeba ujauzito ambao ulikuwa ukiharibika mara kwa mara," amesema Kamanda Banga.

Kamanda Banga amesema upelelezi wa shauri hilo unaendelea kukamilishwa na kwamba mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili mara taratibu za kisheria zitakapokamilika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here