Magazeti leo Februari 3,2026

Mkuu wa Pwani, Abubakar Kunenge, ameipongeza Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Pwani kwa kuiwezesha Serikali kufidiwa kiasi cha shilingi milioni 707 baada ya kumalizika kwa mashauri nane (8) ya uhujumu uchumi yaliyohusisha uharibifu wa miundombinu ya umeme na reli ya SGR mwaka 2025.
Alitoa pongezi hizo Februari 2, 2026, wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini kwa Mkoa wa Pwani, yaliyofanyika katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kibaha mkoani humo.

Aidha, aliipongeza Mahakama kwa mchango wake katika kukuza uchumi na kuunga mkono utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ikiwemo kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kupitia kupunguza migogoro ya ardhi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here