Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Samuel Malecela, amekemea vikali tabia ya kuwatukana Viongozi wa Dini, akieleza kuwa ni kitendo cha kukosa adabu, maadili na ustaarabu ambacho hakipaswi kuvumiliwa katika jamii.
Malecela amesema hakuna sababu wala kisingizio chochote kinachoweza kuhalalisha matusi dhidi ya Viongozi wa Dini, akisisitiza kuwa tofauti za maoni hazimpi mtu haki ya kufokea, kudhalilisha au kuwavunjia heshima watu wanaoheshimika katika jamii.
Akizungumza kwa msisitizo, Malecela amewataka watu wanaojiita Makada kuacha kuvaa mashati ya kijani na kuwadhalilisha wenzao wakidhani hawatasemwa, akibainisha wazi kuwa hatounga mkono tabia hiyo hata kidogo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo

















