TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, jana Februari 4, 2026, imekutana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.
Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa ulihusisha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, ambapo Tume ilijadili chanzo cha matukio hayo, athari zake kwa watu, mali na miundombinu pamoja na mapendekezo ya kuyazuia yasijirudie.Tume inaendelea kukutana na makundi mbalimbali yakiwemo waathirika wa matukio hayo katika mikoa tofauti, ambapo Dodoma shughuli zinafanyika katika Ukumbi wa Takwimu, Iringa katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo na Shinyanga katika Ukumbi wa Manispaa ya Kahama.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo



















