Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025,tarehe 6 Februari, 2026 imeendelea kukutana na viongozi na wananchi wa makundi mbalimbali, ambapo leo imekutana na Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda.
Kikao hicho cha pamoja kati ya Tume na Waziri Mkuu Mstaafu kililenga yaliyojiri katika kipindi cha uchaguzi Oktoba 29, ambapo vitendo vya uvunjifu wa amani na uharibifu wa miundombinu ulitokea .
Kwa sasa Tume bado inaendelea kukusanya taarifa hizo kwa lengo la kuziwasilisha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya utekelezaji wa kudhibiti vitendo hivyo visitokee tena nchini.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo











