Rais Dkt.Samia afanya mabadiliko ya muundo wa wizara na kuteua viongozi mbalimbali leo

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya muundo wa Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji na Wizara ya Nishati kwa Wizara hizo kuwa na Makatibu Wakuu wawili kila moja, hatua inayolenga kuimarisha ufanisi wa utendaji na uhakika wa uongozi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 6,2026 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi wa viongozi umefanyika kama ifuatavyo:

Wakuu wa Mikoa


Kanali Donald William Msengi ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, akichukua nafasi ya Kanali Patrick Kenan Sawala ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Makatibu Wakuu

Dkt. Tausi Mbaga Kida ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango.

Balozi Waziri Rajab Salum ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda na Biashara, akichukua nafasi ya Dkt.Hashil Twaib Abdallah ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here