Magazeti leo Aprili 16,2026

Serikali imeweka bayana dhamira yake ya kuendeleza ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali nchini, kwa lengo la kuhakikisha shughuli za mashirika hayo zinaendana na vipaumbele vya Taifa na kuchochea maendeleo jumuishi kwa wananchi.
Hayo yalibainishwa na Kaimu Kamishna Msaidizi Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Joseph Haule, wakati akifungua warsha ya siku moja yenye lengo ya kujenga uelewa na kubadilishana uzoefu na mashirika yasiyo ya kiserikali, iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Edema, mkoani Morogoro.

Alisema warsha hiyo itawezesha washiriki kuelewa kuhusu ushirikiano kati ya Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali hapa nchini ili kuimarisha ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kijamii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here