Serikali imeweka bayana dhamira yake ya kuendeleza ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali nchini, kwa lengo la kuhakikisha shughuli za mashirika hayo zinaendana na vipaumbele vya Taifa na kuchochea maendeleo jumuishi kwa wananchi.
Hayo yalibainishwa na Kaimu Kamishna Msaidizi Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Joseph Haule, wakati akifungua warsha ya siku moja yenye lengo ya kujenga uelewa na kubadilishana uzoefu na mashirika yasiyo ya kiserikali, iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Edema, mkoani Morogoro.Alisema warsha hiyo itawezesha washiriki kuelewa kuhusu ushirikiano kati ya Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali hapa nchini ili kuimarisha ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kijamii.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo
















