Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kaspar Mmuya ameagiza Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoani Njombe kumkabidhi Charnjeet Singh Sahota hati ya hakimiliki ya Kiwanja Na. 75 Kitalu P mjini Makambako baada ya kubainika kuwa ndiye mmiliki halali wa eneo hilo.
Mmuya alitoa maagizo hayo Mei 9, 2026 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Polisi Makambako kufuatia mgogoro wa muda mrefu wa ardhi uliodaiwa kuhusisha watu waliotaka kujimilikisha eneo hilo kinyume cha sheria.Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Halmashauri ya Mji Makambako, Flaviana Mamkwe, Charnjeet alirithi eneo hilo kutoka kwa baba yake aliyelinunua kihalali miaka iliyopita.
Ziara ya Mmuya mkoani Njombe imelenga kusikiliza kero za ardhi, kukabidhi hati za hakimiliki na kuhamasisha wananchi kulipa kodi ya pango la ardhi.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo

















