Mfanyabiashara Rostam Aziz amewataka Watanzania kuacha mtazamo hasi dhidi ya Wakenya, akisema ushindani usio na tija unaweza kudhoofisha fursa za kiuchumi za kikanda.

Akizungumza Mei 4, 2026 katika kongamano la biashara kati ya Tanzania na Kenya lililofanyika Julius Nyerere International Convention Centre jijini Dar es Salaam, Rostam Aziz alisema kuna haja ya kujenga ushirikiano badala ya kuendeleza mitazamo ya hofu kuhusu ajira na uwekezaji.
Pia aliwataka Wakenya kuepuka kufurahia changamoto zinazoikumba Tanzania, akisisitiza umuhimu wa kuheshimiana katika uhusiano wa kikanda.
Kongamano hilo lilihudhuriwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na Rais wa Kenya William Samoei Ruto pamoja na wadau wa biashara.
“Umoja ni nguvu, tunahitaji mfumo mmoja wa biashara unaofanya kazi kwa kasi na ufanisi,” alisema Aziz.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo

















