Mbunge wa Viti Maalum Vyuo Vikuu, Selina Kingalame, amesema licha ya serikali kuongeza bajeti ya mikopo ya elimu ya juu hadi kufikia Sh bilioni 917, bado mahitaji ya wanafunzi ni makubwa.
Akichangia hotuba ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mei 07 bungeni jijini Dodoma, Kingalame amesema baadhi ya wanavyuo wanaopata mikopo hulazimika kutumia fedha za kujikimu maarufu kama 'boom' kulipa ada kutokana na kiwango cha fedha wanachopata kutokutosha.
Ameiomba serikali kuongeza uwezo wa utoaji wa mikopo ili kuwasaidia wanafunzi wa elimu ya kati na juu kumudu gharama za masomo na maisha ya chuoni.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




















