PWANI-Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Mei 22, 2026 huko maeneo ya Tungutungu, Mapinga, Wilayani Bagamoyo, limeokoa jumla ya ng’ombe 28 kati yao ng’ombe 13 ni mali ya Fadhili Ally Ngabilo mkazi wa Kwa Makocho, Kata ya Mandela wilayani Chalinze.
Mei 16, 2026 Bw. Fadhili Ngabilo aliripoti katika kituo cha Polisi Chalinze kuibiwa jumla ya ng’ombe 18 na mbuzi 05 ambapo Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kupitia Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo (STPU) walianza ufuatiliaji mara moja mpaka Mei, 22 majira ya saa 3:00 asubuhi walipofanikiwa kuwapata ng’ombe 28 wakiwemo ng’ombe 13 kati ya 18 walioibiwa Chalinze wakiwa kwenye zizi la mfanyabiashara mmoja wa nyama.Kati ya ng’ombe wengine 15 waliokutwa nyumbani kwa mtuhumiwa, ng’ombe 5 walitambulika na ng’ombe 4 mahojiano yanaendelea.
Aidha ilibainika mtuhumiwa huyo huwa anachinja ng’ombe wa wizi nyumbani hapo kisha kuuza nyama kwenye bucha yake.


