KIGOMA-Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limetoa wito kwa vijana kata ya Buhigwe, Wilaya ya Buhigwe, Mkoa wa Kigoma kushiriki kuimarisha usalama maeneo wanayoishi kwa kufanya doria kupitia vikundi vya ulinzi shirikishi.
Wito huo umetolewa Mei 9,2026 na Mkaguzi wa Polisi (INSP) Mhadham Miyonga wakati akitoa elimu ya umuhimu wa vikundi vya ulinzi shirikishi katika kuimarisha usalama ambapo amewataka vijana kushiriki kuimarisha usalama maeneo wanayoishi kwa kufanya doria kupitia vikundi vya ulinzi shirikishi, wasione jukumu hilo ni la kundi la wazee ndani ya jamii bali hata wao wanawajibu kushiriki kuimarisha usalama.
INSP Miyonga amewataka vijana hao kuendelea kulinda amani ndani ya jamii kwa kutoa taarifa za wahalifu na kutoshiriki vitendo vya uvunjifu wa amani.
Pamoja na hayo amewataka vijana hao kutojihusisha na matumzi ya dawa za kulevya kwa usalama wa afya zao.
