MUFINDI-Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba amefanikisha kulipwa papo hapo madeni ya wananchi wa Mufindi yenye thamani ya sh. milioni 5.6 kutokana kazi walizofanya kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi.
Madeni hayo ni ya kikundi cha vijana cha Ibantu ambao walikuwa wanadai sh.milioni 3.9 na fundi ujenzi wa vyoo ambaye alikuwa anadai sh. milioni 1.5 tangu mwaka 2022. Kikundi cha Ibantu kilipewa tenda ya kufyatua matofali 15,600 ambayo waliikamilisha.
Hayo yamejiri leo Jumamosi, Mei 2, 2026 wakati Waziri Mkuu akisikiliza kero za wananchi wa Igowole, wilayani Mufindi, mkoani Iringa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Igowelo ambako pia alisikiliza kero za wananchi.


