Zaidi ya wahitimu 450 wa Klabu ya Kupinga Rushwa Mkoa wa Temeke kutoka Chuo cha Diplomasia (CFR), Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) wametunukiwa vyeti na kuaswa kusimamia haki, uadilifu, uwajibikaji na kuwa na ujasiri wa kusema ukweli katika mapambano dhidi ya rushwa.
Akizungumza Juni 6, 2026, jijini Dar es Salaam, kwa niaba ya Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Temeke katika mahafali ya kwanza ya wanachama wa Klabu ya Kupinga Rushwa Mkoa wa huo, yaliyofanyika DUCE, Mkuu wa TAKUKURU Kigamboni, Bibiana Bundala, amesema kuwa vita dhidi ya rushwa ni jukumu la kila mwananchi na si la TAKUKURU.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo



















