NA DIRAMAKINI
OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imetoa taarifa kwa umma kuhusu mabadiliko ya tarehe ya Mafunzo Maalum ya Bespoke kwa mawakili wa Serikali.
Mafunzo hayo, ambayo awali yalipangwa kufanyika kuanzia tarehe 22 hadi 24 Juni 2026, sasa yamepangwa kufanyika kuanzia tarehe 15 hadi 17 Julai 2026 katika Kituo cha Mikutano cha AICC, Arusha.Mabadiliko haya yamelenga kuhakikisha ushiriki wa juu na maandalizi bora ya mafunzo hayo muhimu kwa wataalamu wa sheria wa serikali nchini.