Aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, CP Edwin Abraham Mani azikwa nyumbani Bonyokwa

DAR-Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, Kamishna wa Polisi CP Edwin Abraham Mani umezikwa Julai 18, 2026 nyumbani kwake Bonyokwa, Ilala Dar es Salaam.
Katika kutoa salamu za pole kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi DCP Daniel Nyambabe amesema marehemu ameliachia heshima kubwa Jeshi la Polisi. Aliongeza kuwa CP Edwin alifanya kazi kwa weledi mkubwa hadi wakati wa kustaafu kwake.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, Kamishna Mwandamizi wa Polisi SACP Renada Mzinga amesema kuwa ingawa CP Edwin alikuwa amestaafu, alikuwa msaada mkubwa katika kutoa ushauri wa masuala mbalimbali ya kiutendaji ndani ya Jeshi hilo, hasa katika Kamisheni ya Upelelezi.
Aliongeza kuwa marehemu alikuwa mstari wa mbele katika kulinda heshima na weledi wa Jeshi la Polisi na mchango wake katika kupambana na uhalifu ulitambulika.

Maziko hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Edward Mpogolo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh. Albert Chalamila. Pia walihudhuria viongozi wa Jeshi la Polisi pamoja na ndugu, jamaa na marafiki.
Marehemu aliwahi kufanya kazi katika Mikoa na vitengo mbalimbali vya Jeshi la Polisi. Mara ya mwisho alihudumu kama Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, madaraka aliyostaafu nayo mwaka 1996.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here