Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Profesa Raphael Chibunda, amesema panya Magawa, aliyefunzwa na SUA kwa kushirikiana na shirika la APOPO, ameacha historia kubwa nchini Cambodia baada ya kusaidia kugundua mabomu ya ardhini na hatimaye kujengewa mnara wa kumuenzi katika mji wa Siem Reap.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Agosti 31,2026, Profesa Chibunda amesema panya wanaotumika katika mradi huo ni panya wa asili wa Tanzania, ambao awali walikamatwa katika milima ya Uluguru mkoani Morogoro na sasa wanaendelea kuzalishwa na kufundishwa katika kituo hicho.
Amesema SUA imeweka mfumo maalumu wa kuwahudumia panya hao katika hatua mbalimbali za maisha yao, kuanzia kuzaliwa, mafunzo hadi kustaafu.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























