Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi wa Polisi Salim Morcase jana Septemba 2, 2026 amewataka maafisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wilayani Bagamoyo kufanya kazi kwa weledi na uadilifu.
Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na askari katika kikao kazi ambapo amewataka askari kuzingatia mwenendo mwema wa utendaji kazi wenye kuzingatia nidhamu, haki, weledi na uadilifu ili kutoa huduma bora kwa wateja na jamii wanayoihudumia.
Akizungumza katika kikao hiko, Kamanda Morcase amewataka askari kuwa na tabia njema na nidhamu wanapokuwa wanawahudumia wateja pasipo kujali hali zao na masharti yaliyo nje ya utaratibu wa Haki Jinai ili kuepusha malalamiko yanayoepukika na kuleta tija katika kutekeleza majukumu yao.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




















