Wizara ya Madini inawaalika wanafunzi wa Vyuo Vikuu kote nchini kushiriki katika shindano la kubuni teknolojia mbadala zinazoweza kupunguza au kuondoa matumizi ya kemikali ya zebaki na matumizi ya matimba katika uchimbaji mdogo.Hii ni nafasi ya kuonesha uwezo wako wa ubunifu, kutoa suluhisho zenye manufaa kwa mazingira na jamii, na kuchangia maendeleo ya sekta ya madini nchini Tanzania.
Usikose fursa ya kubadili wazo lako kuwa sehemu ya mabadiliko yenye athari chanya.Shiriki sasa!.