Tanzania imepata nafasi 150 za ufadhili wa masomo ya elimu ya juu nchini Algeria kwa mwaka 2026, zikilenga wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya sayansi.
Akizungumza na waandishi wa habari Septemba 11 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda alisema kuwa Aljeria itagharamia ada za masomo huku Tanzania ikitoa fedha za kujikimu kupitia mpango wake wa Samia Scholarship.
Samia Scholarship imetajwa kuwa ni mpango maalum wa serikali uliowekwa kutoa ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika mitihani ya kidato cha Sita kwenye masomo ya sayansi, kwa lengo la kukuza wataalam wa ndani na kuongeza fursa za elimu bila kikwazo cha kipato.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo






















