Magazeti leo Septemba 12,2026

Tanzania imepata nafasi 150 za ufadhili wa masomo ya elimu ya juu nchini Algeria kwa mwaka 2026, zikilenga wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya sayansi.
Akizungumza na waandishi wa habari Septemba 11 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda alisema kuwa Aljeria itagharamia ada za masomo huku Tanzania ikitoa fedha za kujikimu kupitia mpango wake wa Samia Scholarship.

Samia Scholarship imetajwa kuwa ni mpango maalum wa serikali uliowekwa kutoa ufadhili wa masomo ya elimu ya juu kwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika mitihani ya kidato cha Sita kwenye masomo ya sayansi, kwa lengo la kukuza wataalam wa ndani na kuongeza fursa za elimu bila kikwazo cha kipato.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here