Magazeti leo Julai 4,2026

Wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuhakikisha wanapata pembejeo za kilimo kwa wakati, hatua ambayo wamesema itawawezesha kujiandaa mapema kwa msimu wa uzalishaji.
Wakulima hao wameanza kupokea pembejeo mbalimbali ikiwemo dawa za maji na dawa ya unga (Sulphur), huku wakieleza kuwa upatikanaji wake kwa wakati ni ishara ya dhamira ya Serikali ya kuboresha sekta ya kilimo.

Mkulima wa korosho kutoka kijiji cha Nansinji, Rashid Hamid maarufu kwa jina la Mkapa, alisema wakulima wanathamini juhudi za Rais Samia za kuhakikisha pembejeo zinapatikana licha ya changamoto mbalimbali zinazoikabili dunia.

"Sisi wakulima tunatambua jitihada za Rais Samia kutupatia pembejeo. Hatukutarajia kupata kwa urahisi kutokana na changamoto za upatikanaji wa bidhaa duniani zilizotokana na migogoro mbalimbali. Kupatikana kwa dawa hizi ni jambo la kutia moyo na linaonyesha namna Rais anavyowathamini na kuwapambania wakulima," alisema.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wa ziara ya Afisa Tarafa, Emmanuel Shilatu, aliyefanya ukaguzi wa mwenendo wa ugawaji wa pembejeo ili kujiridhisha kuwa zoezi hilo linafanyika kwa ufanisi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here