ZANZIBAR-Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC),Mhandisi Machibya Shiwa ametembelea Banda la TRC katika maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayoendelea kisiwani Zanzibar.
TRC inashiriki katika tamasha hilo kwa lengo la kuelimisha wananchi kuhusu huduma zinazotolewa na shirika, miradi ya kimkakati inayotekelezwa, pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo katika ushoroba wa reli.
Katika banda hilo, wananchi na wadau mbalimbali wanaendelea kupata elimu na taarifa kuhusu huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo, huduma za kukata tiketi, pamoja na fursa zinazotokana na maendeleo ya sekta ya reli nchini.
