Rais Dkt.Mwinyi atoa wito kwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemtaka Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Meja Jenerali Mbaraka Naziad Mkeremy kutumia nafasi yake kuimarisha diplomasia ya uchumi hususan katika kuvutia uwekezaji, kukuza biashara na kuongeza watalii kutoka Malaysia wanaotembelea Zanzibar.
Ameyasema hayo leo Agosti 17,2026 alipokutana na Balozi Mkeremy aliyefika Ikulu Zanzibar kuaga na kupokea maelekezo kabla ya kuelekea katika kituo chake kipya cha kazi nchini Malaysia.

Mheshimiwa Rais amesisitiza umuhimu wa kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar katika utalii, hoteli na makaazi, uvuvi, mafuta na gesi pamoja na maeneo mengine ya Uchumi wa Buluu.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amemtaka Balozi Mkeremy kuimarisha ushirikiano wa Zanzibar na Malaysia katika elimu, ikiwemo kuongeza fursa za ufadhili wa masomo na ushirikiano baina ya vyuo vikuu.
Naye Balozi Mkeremy amesema,amepokea maelekezo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi katika utekelezaji wa majukumu yake nchini Malaysia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here