Yanga SC yatwaa Ngao ya Jamii ikiichapa Simba SC bao 1-0

NA DIRAMAKINI

MABINGWA wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Yanga SC ya jijini Dar es Salaam wametwaa Ngao ya Jamii baada ya kuwachapa watani zao wa jadi, Simba SC ya jijini Dar es Salaam bao 1-0.
Ni kupitia mtanange wa aina yake ambao ulikuwa na mvuto mkubwa uliopigwa leo Agosti 12, 2026 katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Bao pekee la mchezo huo limefungwa na mshambuliaji, Albert Kangwanda akimalizia krosi iliyochongwa na beki wa kushoto, Chedrack Boka.
Yanga na Simba zimekutana katika mchezo wa Ngao ya Jamii baada ya kumaliza msimu uliopita zikiwa na mataji mawili tofauti. Yanga waliibuka mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania, huku Simba wakitwaa Kombe la CRDB Federation Cup. 

Mchezo huu umekuwa kipimo cha kwanza cha nguvu za timu hizo kuelekea msimu mpya wa 2026/27, huku Yanga ikionekana kuwa na nguvu zaidi.
Katika Ngao ya Jamii ya mwaka uliopita, Yanga iliifunga Simba 1-0, bao likifungwa na Pacome Zouzoua.Aidha,Simba SC imeingia kwenye mchezo ikiwa na sura mpya na kocha mpya, Steve Barker huku Yanga nayo ikianza ukurasa mpya chini ya Manqoba Mngqithi wote kutoka nchini Afrika Kusini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here