Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) umetakiwa kuongeza ushirikiano na Sekta Binafsi pamoja na wadau wengine ili kupata fedha zinazohitajika kukamilisha miradi ya maji katika vijiji 1,575 ambavyo bado havijafikiwa na huduma hiyo nchini.
Ushauri huo umetolewa Septemba 9, 2026 Jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na mlezi wa RUWASA, Bi. Rose Ambrose, wakati akifungua kikao kazi cha siku tatu cha Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti pamoja na Mameneja wa RUWASA wa Mikoa na Wilaya.Amesema kuwa RUWASA inakabiliwa na mahitaji ya Sh trilioni 5.1 kwa ajili ya kukamilisha utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji vilivyosalia, wakati fedha zilizopo ni Sh trilioni 2.06, hivyo kuna pengo la takribani Sh trilioni 3.











Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo