Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kusogeza huduma na elimu kuhusu viwango, ubora na usalama wa bidhaa karibu na wananchi kupitia Kliniki ya Viwango, hatua inayolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo na kuwawezesha wafanyabiashara kuzingatia matakwa ya viwango.
Akizungumza wakati wa Kliniki hiyo inayoendelea Kariakoo na Mwenge Jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Salum Yusuph, kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Kinondoni ameipongeza TBS kwa kuendelea kuwafikishia wananchi huduma hizo, akisema zina mchango mkubwa katika kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa, kusambazwa na kuuzwa nchini zinakidhi viwango vinavyotakiwa.
Yusuph amesema huduma zinazotolewa na TBS, ikiwemo upimaji, ukaguzi, usajili wa bidhaa na majengo pamoja na elimu kwa umma, ni muhimu katika kulinda afya za wananchi na kujenga imani katika bidhaa zinazouzwa sokoni.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




























