NA DIRAMAKINI
MUME wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mheshimiwa Hafidh Ameir Hassan amefariki dunia.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Septemba 7,2026 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati akitangaza taarifa ya msiba wa Mhe. Hafidh Ameir Hassan ambaye amefariki leo.
Kifo hicho kimetokea majira ya saa mbili asubuhi katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa moyo.
Aidha, mipango ya mazishi na maziko inaendelea kufanyika nyumbani Kizimkazi Zanzibar.
Tags
Breaking News
Dr Samia Suluhu Hassan
Habari
Hafidh Ameir Hassan
Msiba wa Taifa
Mwenza wa Rais Samia
