NAIBU WAZIRI NDEJEMBI AONYA VITENDO VYA RUSHWA KWA WATUMISHI WA IDARA YA ARDHI MKURANGA

NA VERONICA MWAFISI

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi ameonya vitendo vya rushwa vinavyofanywa na baadhi ya watumishi wa Idara ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga wakati wa kikao kazi chake na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji. 

Akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga katika kikao kazi chake na watumishi hao, Mhe. Ndejembi amewataka kujirekebisha na kufanya kazi kwa uadilifu na weledi ili kuondoa migogoro isiyo ya lazima inayosababishwa na utendaji kazi wao usioridhisha.

Ameongeza kuwa, watumishi wa Idara hiyo ya ardhi wakiendelea na utamaduni wa kufanya kazi kwa kuweka maslahi binafsi mbele wataipotezea Serikali mapato na kuwanyima haki wananchi wa Mkuranga kupata maendeleo yanayotokana na kodi itayokusanywa na Serikali katika Halmashauri hiyo.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi chake na watumishi hao wilayani Mkuranga chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji. 
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Khadija Ali akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi kuzungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akisikiliza hoja ya mmoja wa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa Halmashauri hiyo chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Bi. Jessy Mpangala akiwasilisha changamoto ya kiutumishi inayomkabili kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji. 

Akisisitiza uadilifu kwa watumishi hao, Mhe.Ndejembi amewataka wabadilike kwa sababu wamekuwa wakilalamikiwa kuwaonea wananchi kwa kuwaomba rushwa na kutowashauri vizuri kwenye masuala yanayohusu umiliki wa ardhi.

“Nimeambiwa hapa Mkuranga hata mimi nikihitaji shamba natakiwa kuwa na kitu kidogo cha kuwapatia watumishi wa Idara ya ardhi ambao wameweka maslahi yao binafsi mbele, na wala sitaki kumtaja mtu mmoja mmoja hapa zaidi ya kuwasisitiza mbadilike”, Mhe. Ndejembi amefafanua.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akiwahimiza watumishi wa Halmashauri ya Wilaya Mkuranga kutumia mfumo wa SEMA NA WAZIRI WA UTUMISHI kwa kuwasikilizisha makala fupi ya picha za mwendo (video clip) inayotoa muongozo wa namna ya kutumia mfumo huo, wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri hiyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Mkuranga Bi. Mwantum Mgonja akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya halmashauri yake kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na Watumishi wa Halmashauri hiyo chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Kuhusiana na migogoro inayoibuka, Mhe. Ndejembi amewataka Watumishi wa Idara hiyo kuwa watatuzi wa migogoro badala ya kuwa chanzo cha migogoro.

Mhe. Mhe. Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma wa Halmashauri hiyo, ikiwa ni pamoja na kukagua utekelezaji wa Mpango wa Kuzinusuru Kaya Maskini unaoratibiwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news