Orodha ya wanafunzi waliopangiwa kwenda Shule Kidato cha Tano,Vyuo vya Ualimu na Ufundi Stadi 2022

 NA GODFREY NNKO


OFISI ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Baraza la Mitihani la Tanzania imekamilisha zoezi la uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Tano katika shule za sekondari, Vyuo vya Ualimu na Vyuo vya Elimu ya Ufundi vya Serikali Mwaka 2022.

Zoezi hilo limefanyika kwa kuzingatia takwimu za matokeo ya wanafunzi waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne Mwaka 2021 kutoka Tanzania Bara.

Hayo yamesemwa leo Mei 12,2022 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI),Mhe. Innocent Bashingwa (MB) wakati akitangaza matokeo hayo ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Amesema,watahiniwa katika mtihani wa Kidato cha Nne kwa mwaka 2021 waliopata Daraja la I hadi III walikuwa 173,422 wakiwemo wasichana 75,056 na wavulana 98,366.

Kati ya wanafunzi hao, wanafunzi wenye sifa ya kujiunga na Kidato cha Tano, vyuo vya Ualimu na vyuo vya Ufundi ni 167,515 wakiwemo wasichana 71,433.

"Idadi hiyo ya wanafunzi wenye sifa imejumuisha wanafunzi wenye mahitaji Maalum 508 wakiwemo wasichana 217 na wavulana 291. Hii ni ongezeko la wanafunzi 19,388 kwa kulinganisha na wanafunzi 148,127 waliokuwa na sifa kwa mwaka 2021.


Mheshimiwa Bashungwa amesema, wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ualimu na Vyuo vya Elimu ya Ufundi mwaka 2022, ni kutoka Shule za Serikali, zisizo za Serikali, watahiniwa wa kujitegemea waliofanya mtihani kupitia Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima waliokidhi vigezo na waliosoma Nje ya nchi ambao matokeo yao yamefanyiwa ulinganifu wa Baraza la Mtihani Tanzania (NECTA).

"Wanafunzi 153,219 wakiwemo wasichana 67,541 na wavulana 85,678 sawa na asilimia 91.8 ya wenye sifa, wamechaguliwa kujiunga na Shule za sekondari Kidato cha Tano, Vyuo vya Ualimu na Vyuo vya Elimu ya Ufundi mwaka, 2022 katika mchanganuo ufuatao;

"Wanafunzi 90,825 wakiwemo wasichana 43,104 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano katika Shule za Sekondari 499 za Serikali zikiwemo Shule mpya 22 za Serikali zilizoanza mwaka, 2022.

"Kati ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha Tano, wapo wanafunzi wenye Mahitaji Maalum 481 ambao kati yao wasichana ni 204. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano, wanafunzi 41,401 wakiwemo wasichana 17,390 watajiunga kusoma tahasusi za Sayansi na Hisabati na wanafunzi 49,133 wakiwemo wasichana 25,508 watajiunga kusoma tahasusi za masomo ya Sanaa, Lugha na Biashara;

Fani mbalimbali

"Wanafunzi 1,880 wakiwemo wasichana 757 wamechaguliwa kujiunga na fani mbalimbali katika Vyuo 03 vya Elimu ya Ufundi ambavyo ni Chuo cha Ufundi cha Arusha (ATC), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na Chuo cha Usimamizi na Maendeleo ya Maji (WDMI),"amefafanua Mheshimiwa Bashungwa.

Amesema,wanafunzi 2,294 wakiwemo wasichana 1,127 wamechaguliwa kujiunga na Vyuo vya Afya ngazi ya Stashahada;

Pia amesema,wanafunzi 2,674 wakiwemo wasichana 1,366 wamechaguliwa kujiunga na Vyuo vya Ualimu ngazi ya Stashahada ya Sayansi, Hesabu na TEHAMA.

OFISI YA RAIS - TAMISEMI

UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI

CHOOSE SELECTION VERSION
SELECTION DETAILS
Please, browse using the hierarchy on the left
EXAMINATION CENTER 
CANDIDATE NAME
SEX
AGE
HOME COUNCIL
SELECTION
JOINING INSTRUCTIONSClick for joining instructions (ONLY IF ALREADY AVAILABLE!)
Wanafunzi 6,457 wakiwemo wasichana 3,168 wamechaguliwa kujiunga na Astashahada ya Elimu Maalum, Awali, Michezo, Msingi na Ualimu wa Shule zinazofundisha kwa kutumia Lugha ya Kiingereza (English Medium).

Amesema,wanafunzi 49,089 wakiwemo wasichana 18,019 wamechaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za Astashahada na Stashahada (Certificate and Ordinary Diploma) katika Vyuo vya Elimu ya Ufundi vinavyosimamiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTVET).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

1 Comments

Previous Post Next Post

International news