BREAKING NEWS: Mtutura Abdallah Mtutura ang'atuka CCM, asajiliwa ACT Wazalendo baada ya maamuzi ya jana

SIKU moja baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutangaza majina ya wateule ambao watapeperusha bendera ya chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 28, mwaka huu, joto limezidi kupanda kwa wanachama ambao hawakukidhi vigezo.

 Kutokana na hatua hiyo, leo Agosti 21, 2020, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tunduru (na baadaye Tunduru Kusini) kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM (2007-2015), Mtutura Abdallah Mtutura amehama CCM na kujiunga na ACT Wazalendo, anaripoti Mwandishi Wetu...

 
 Mtutura amekabidhiwa kadi ya ACT Wazalendo na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu katika Ofisi ya ACT Wazalendo Tunduru mkoani Ruvuma. Kwa kina zaidi, ungana nasi kupitia www.diramakini.co.tz taarifa kamili zitakujia punde

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news