Profesa Mkenda, Ndakidemi,Dkt.Kimei, Tarimo,Mafuwe,Thadayo,Kilango,Mathayo David Mathayo watoboa siri

 Pia wenyeviti wa Kitaifa watatu wa vyama vya siasa akiwemo Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ataunguruma Jimbo la Hai, huku Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Agustino Lyatonga Mrema wakiunguruma Jimbo la Vunjo.

WAGOMBEA wa  ubunge  kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika majimbo nane kati ya tisa ya uchaguzi yaliyopo Mkoa wa Kilimanjaro wamechukua fomu kuomba kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kupeperusha bendera ya chama hicho, inaripoti www.diramakini.co.tz

Msimamuzi wa Uchaguzi, Jimbo la Hai, Yohana Sintoo akimkabidhi fomu ya kuomba kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kugombea ubunge katika jimbo hilo, mgombea ubunge kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Saashisha Mafuwe. Picha na www.diramakini.co.tz

Waliochukua fomu hizo ni pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt.Charles Kimei anayegombea Jimbo la Vunjo,Profesa Adolf Mkenda Jimbo la Rombo,Profesa Patrick Ndakidemi Jimbo la Moshi Vijiji, Priscus Tarimo  Jimbo la Moshi Mjini, Saashisha Mafuwe Jimbo la Hai,Joseph Thadayo Jimbo la Mwanga, Anna Kilango Jimbo la Same Mashariki na Mathayo David Mathayo  Jimbo la Same Magharibi.

Mgombea Ubunge Jimbo la Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi, aliyevaa shati la maua, akijadiliana jambo na mgombea ubunge Jimbo la Vunjo,Dkt.Charles Kimei baada ya kuchukua fomu kwa msimamizi wa uchaguzi leo. Picha na www.diramakini.co.tz


Wagombea hao kwa nyakati tofauti wamejitokeza katika ofisi za halmashauri kwa wasimamizi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua fomu hizo, na kila mmoja mbali na kushukuru kwa kuaminiwa na chama hicho, wameieleza www.diramakini kuwa, wanakwenda kupata ushindi mkubwa na wa kishindo.

Katika Mkoa wa Kilimanjaro, mbali na CCM, vyama vingine  ambavyo wagombea wamejitokeza kuomba kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, katika majimbo mbalimbali,kugombea nafasi ya Ubunge ni kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ACT-Wazalendo, CUF, NCCR Mageuzi,TLP na SAU.
 

 
Saashisha Mafuwe, mgombea Ubunge Jimbo la Hai. Video na www.diramakini.

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Moshi Mjini, Michael Mwandezi, akimuelekeza mgombea ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Priscus Tarimo wakati alipokwenda kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho leo. Picha na www.diramakini.co.tz
 
Dkt.Charles Kimei, mgombea ubunge Jimbo la Vunjo. Video na www.diramakini.co.tz
Priscus Tarimo, Mgombea     Jimbo la Moshi Mjini. Video na www.diramakini.co.tz
Profesa Patrick Ndakidemi, Mgombea ubunge Jimbo la Moshi Vijijini. Video na www.diramakini.co.tz
Joseph Tadayo, Mgombea ubunge Jimbo la Mwanga. Video na www.diramakini.co.tz
Dkt.Mathayo David Mathayo, Mgombea Ubunge Jimbo la Same Magharibi. Video na www.diramakini.co.tz
Anna Kilango Malecela, Mgombea Ubunge Jimbo la Same Mashariki. Video na www.diramakini.co.tz

Pia kwenye uchaguzi huu, Kilimanjaro wenyeviti watatu wa Kitaifa wa vyama vya siasa, Ni miongoni mwa wagombea waliojitokeza kugombea ubunge mkoani Kilimanjaro, ambapo Mwenyekiti wa CHADEMA, Freemani Mbowe, ataunguruma jimbo la Hai, huku Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na Agustino Lyatonga Mrema wakiunguruma Jimbo la Vunjo.

Karibu! Tovuti hii ya www.diramakini.co.tz imesajiliwa rasmi na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kupewa leseni namba TCRA/OCS-BL/0197/2020 chini ya Diramakini Business Limited iliyosajiliwa nchini Tanzania kwa ajili ya kukuhabarisha, kukuelimisha na kukupasha habari mbalimbali toka ndani na nje ya nchi. Je? Una habari,maulizo au tangazo, unataka kutupa ufadhili? Tuwasiliane; diramakini@gmail.com Asante.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news