![]() |
| Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Rajab Mabele
akizungumza wakati Makatibu Wakuu na Naibu Katibu Wakuu kutoka Wizara
mbalimbali wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi
walipotembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ikulu Chamwino jijini
Dodoma jana.Naye
Mkurugezi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Rajab Mabele alisema
kuwa, ujenzi wa Ikulu unaendelea kwa kasi kutokana na ushirikiano mzuri
uliopo kati ya JKT na TBA ambao ni wasimamizi wa mradi huo. |
“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuendelea kutuamini na kutupa kazi hii ya ujenzi wa Ikulu hapa Chamwino,”alisema.
![]() |
Akifafanua alisema kuwa, miradi iliyotolewa na wizara mbalimbali imeiwezesha SUMA JKT kununua mitambo, vifaa vya kisasa, magari na hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji.
Aliongeza kuwa, SUMA JKT itaendelea kufanya kazi usiku na mchana kukamilisha mradi huu kwa wakati ambapo katika kutunza mazingira wamepanda miti zaidi ya 5,600 katika eneo hilo.
Tags
Habari



