Zuchu atwaa tuzo ya mwanamuziki bora Afrika

Msanii chipukizi na Mtanzania, Zuchu Otuman ametwaa tuzo ya msanii bora chipukizi Afrika kutoka African Music Magazine Awards (AFRIMMA), anaripoti Mwandishi Diramakini.

Zuchu ambaye ni mtoto wa malkia wa nyimbo za taarabu nchini, Hadija Kopa hii ni tuzo yake ya kwanza ya Kimataifa tangu ajiunge na lebo ya WCB Aprili 8, 2020 na tayari kazi zake zimeendelea kufanya vizuri ndani na nje ya Tanzania.

Miongoni mwa nyimbo za Chuchu zinazobamba zaidi kwa sasa ni pamoja na Wana, Raha, Nisamehe, Kwaru, Mauzauza, Shindua, Hakuna Kulala na Asua ambayo amemshirikisha Mbosso pia kutoka WCB
.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news