Jumla ya watoto 252 wamepata huduma za upasuaji wa moyo kupitia ushirikiano uliopo kati ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Shirika la Save a Child’s Heart (SACH) la nchini Israel hatua iliyosaidia kuokoa maisha yao.

Kati ya watoto hao 170 walifanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalumu zilizofanywa hapa nchini na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa SACH huku watoto 82 wakipelekwa nchini Israel kwa matibabu zaidi.
Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa JKCI, Dkt. Naizihijwa Majani alipokuwa akizungumza na Balozi wa Israel nchini Tanzania Mhe. Gideon Behar alipotembelea taasisi hiyo kujionea huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na uwekezaji uliofanywa na serikali ya Tanzania katika matibabu ya moyo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























