Aina mpya ya Coronavirus inayosambaa kwa kasi yagundulika Botswana, Gambia, Zambia na Kenya

Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO) limesema kuwa, aina mpya ya virusi vya Corona vinavyosambaa kwa kasi kuliko aina ya kwanza imegunduliwa katika nchini za Botswana, Zambia, Gambia na Kenya.
Mkurugenzi wa shirika hilo barani Afrika, Matshidiso Moeti amesema kwamba, virusi hivyo vinasambaa kwa kasi kutokana na safari nyingi za watu kote barani Afrika.

Katika kikao na waandishi wa habari, Matshidiso amesema kwamba, mpango wa COVAX, wa shirika hilo unaolenga kutoa chanjo kwa nchi maskini, unapanga kutoa dozi milioni 600 dhidi ya virusi vya Corona kote Afrika ndani ya mwaka huu.

Amesema kwamba, watu milioni 3.3 wameambukizwa virusi vya Corona kote Afrika hadi sasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news