Biashara United yaichapa Gwambina FC 1-0

Biashara United ya mkoani Mara leo Januari 3, 2021 imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gwambina FC,anaripoti Mwandishi Diramakini.
Azam tv/Diramakini.

Mtanange huo ambao umechezwa katika dimba la Gwambina Complex, vijana hao wa Mara wameibuka na ushindi huo kwa bao la Deogratius Mafie alilofunga ndani ya dakika 15.

Aidha, jitihada za wachezaji wa Gwambina FC kuweka kurejesha bao hilo hazikuweza kuzaa matunda hadi dakika ya tisini.

Huu ni mchezo wa kwanza kwa nyota mpya wa Gwambina FC, Mrisho Ngassa kuanza kuitumikia timu yake mpya baada ya kusaini kandarasi kwenye dirisha dogo lililofunguliwa Desemba 16,2020 amnbapo linatarajiwa kufungwa Januari 15, 2021.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news