Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imetoa onyo la mwisho kwa taasisi zote zinazokusanya na kuchakata taarifa binafsi kujisajili kabla ya Aprili 8, 2026 ikibainisha kuwa hatua kali za kisheria zitaanza kuchukuliwa kuanzia Aprili 9,mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari Machi 26, 2026, Mkurugenzi Mkuu wa PDPC, Emmanuel Lameck Mkilia amesema serikali imetoa muda wa kutosha tangu mwaka 2024 kwa taasisi kujisajili ikiwa ni pamoja na kuongeza muda huo mara mbili.
Amesema kuanzia Aprili 9, utekelezaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Sura ya 44 utaanza rasmi, na taasisi au mtu yeyote atakayebainika kutokujisajili atachukuliwa hatua za kisheria.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo





























