KMC FC YAANZA KUJIANDAA DHIDI YA NAMUNGO MECHI ZA VIPORO

Kikosi cha Timu ya KMC FC kimeanzakufanya maandalizi kuelekea katika mchezo wake dhidi ya Namungo utakaopigwa siku ya Alhamisi Februali nne mwaka huu katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam saa 10.00 jioni.
Mchezo huo ni kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ya kuanza kuchezwa kwa mechi zilizoahirishwa (Viporo) ambapo KMC FC ni miongoni mwa Timu ambazo mchezo wake dhidi ya Namungo uliahirishwa.

Aidha hadi sasa maandalizi ya mchezo huo yanaendelea vizuri chini ya Kocha Mkuu John Simkoko pamoja na msaidizi wake Habibu Kondo na kwamba mpango mkakati ni kuhakikisha kuwa KMC FC inafanya maandalizi ya kutosha na hivyo kuondoka na alama tatu muhimu dhidi ya wapinzani Namungo FC.

Imetolewa na Christina Mwagala


Afisa Habari na Mahusiano wa Timu ya KMC FC

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here