TPSC ni taasisi muhimu inayojenga maadili na uwezo wa kiutendaji kwa watumishi-Ndejembi

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ni taasisi muhimu ya kitaaluma yenye jukumu kubwa la kujenga maadili na uwezo wa kiutendaji kwa Watumishi wa Umma waliopo, wanaotarajiwa kuajiriwa na viongozi wateule wajao, hivyo watumishi wake wanapaswa kulinda hadhi ya chuo hicho kwa kufanya kazi kwa bidii, weledi na uadilifu ili kukiwezesha chuo hicho kufikia malengo yake, anaripoti James K.Mwanamyoto-Mtwara.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa kampasi hiyo.

Mhe. Ndejembi amesema hayo, wakati wa ziara yake ya kikazi katika Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa kampasi hiyo.

Mhe. Ndejembi amefafanua kuwa, TPSC ndio chuo pekee kinachojitofautisha na vyuo vingine kwa kutoa mafunzo yanayolenga kujenga maadili bora kwa Watumishi wa Umma waliopo, wanaotarajiwa kuajiriwa ili kuutumikia umma, ikiwa ni pamoja na viongozi wa umma wajao watakaoteuliwa na mamlaka.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa hao.
Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao.

Ameongeza kuwa, Serikali ina dhamira ya kuhakikisha mhitimu kutoka chuo chochote cha ndani au nje ya nchi pindi anapotaka kuingia katika Utumishi wa Umma itamlazimu kupitia TPSC ili kufundishwa maadili na miiko ya Utumishi wa Umma kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yake.
Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika akitoa taarifa ya utekelezaji ya TPSC Kampasi ya Mtwara kwa Mhe. Ndejembi wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa Kampasi ya Mtwara.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akiwasili katika Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa kampasi hiyo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara mara baada ya kuzungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa kampasi hiyo.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika amesema Kampasi ya Mtwara inatoa mafunzo ya muda mfupi na mrefu, kutoa shauri za kitaalam na kufanya tafiti zenye tija ambazo zinatumiwa kutatua changamoto mbalimbali zinazolikabili taifa, hivyo ametoa wito kwa taasisi za umma kuitumia kampasi hiyo kuwajengea uwezo kiutendaji watumishi wao.

Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Mtwara kilizinduliwa mwaka 2009 na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda, ambaye alielekeza TPSC iongeze kampasi mikoani ili kutoa huduma za mafunzo kwa Watumishi wa Umma waliopo na wanaotarajiwa kuajiriwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news