Yanga SC yaigomea TFF mtanange wa leo na watani wao Simba SC


Klabu Yanga SC imesema haitambui Mabadiliko ya muda wa mchezo wao na Watani wao wa Jadi Simba unaochezwa leo kutoka saa 11 Jioni hii hadi saa moja usiku, anaripoti Mwandishi Diramakini.

Taarifa fupi ya Yanga kwa Vyombo vya habari imesema wao watapeleka timu kama ratiba inavyosema saa kumi na moja na kulitaka Shirikisho la soka la TFF, liheshimu kanuni ya 15 inayohusu taratibu za mchezo ambayo inasema mabadiliko yoyote ya muda wa mchezo yatajulishwa ipasavyo kwa pande husika angalau saa 24 kabla ya mchezo husika.

Yanga wanasemaje?

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news