HOSPITALI ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) chini ya menejimenti ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wamefanikuwa kutoa huduma za matibabu bure kwa zaidi ya watu 2,000 kuelekea kilele cha maadhimisho ya wauguzi duniani.
Hospitali hizo pia zimekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika jijini Arusha, yakihusisha shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na utoaji wa huduma za matibabu bure kwa wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho hayo, Dk Saleh Hamisi Mwinchete ambaye ni Daktari Bingwa wa Moyo pamoja na Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya ALMC, alisema maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila tarehe 15 Mei kila mwaka ikiwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa huduma za uuguzi duniani Florence Nightingale, yaliwakutanisha wauguzi kutoka maeneo mbalimbali nchini katika viunga vya Hospitali ya ALMC.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




.jpeg)




.jpeg)





.jpeg)