IGP Simon Sirro afanya mabadiliko Makamanda wa Polisi leo Juni 4,2021

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Simon Sirro leo Juni 4,2021 amefanya mabadiliko ya Makamanda watatu wa Polisi wa mikoa ya Ilala, Shinyanga na Songwe.
Katika mabadiliko hayo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) ACP Debora Magiligimba aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga amehamishiwa Mkoa wa Kipolisi Ilala Kanda Maalumu ya Dar es salaam,akichukua nafasi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Janeth Magomi anayeenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe.

Katika Mabadiliko hayo, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), George Kyando aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news