Rais Samia aongoza kikao cha Kamati Kuu CCM, aelekea Msumbiji mkutano wa dharura SADC

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

KIKAO cha Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimefanyika leo kikiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre, Jijini Dodoma ambacho kilihudhuriwa na viongozi wakuu wa chama hicho akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya (CCM), Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichokutana leo Juni 22,2021 katika Ukumbi wa Jakaya Convention Centre Jijini Dodoma.

Kikao hicho ambacho ni cha kawaida na cha kwanza kwa Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo kimefanyika kujadili masuala mbali mbali ya chama hicho cha CCM.

Kikao hicho kimefanyika baada ya Kikao cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kilichofanyika jana Juni 21,2021 chini ya Mwenyekiti wake Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo huko katika ukumbi wa NEC, White House Jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango, katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma leo Juni 22,2021, alipokua akielekea Nchini Msumbiji kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya SADC unaotarajiwa kuanza kesho.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here