Rais Samia afanya uteuzi wa wakuu wa wilaya wawili


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewateua Suleiman Yusuph Mwenda na Lupakisyo Andrea Kapange kwa Wakuu wa Wilaya mbili tofauti.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu, imesema Mwenda ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

Kabla ya uteuzi huo, Mwenda alikuwa Katibu Msaidizi Idara ya Oganaizesheni ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu Jijini Dodoma na amechukua nafasi ya Kenan Laban Kihongosi ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa UVCCM.

Taarifa hiyo imesema Lupakisyo Andrea Kapange ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu kuchukua nafasi ya Dk. Charles Mhina ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Kabla ya uteuzi huo, Kapange alikuwa Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Tanga.

Uteuzi wa Wakuu hao wa Wilaya umeanza Juni 22, 2021.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here