Serikali kuwachukulia hatua maafisa wanaodanganya kuwasilisha madai ya malimbikizo ya mishahara Ofisi ya Rais-Utumishi

Na Veronica Mwafisi,Kondoa

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Serikali itawachukulia hatua za kinidhamu Maafisa Utumishi wote watakaobainika kuwadanganya Watumishi wa Umma wenye madai ya malimbikizo ya mishahara kuwa wamewasilisha madai yao Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa ajili ya kufanyiwa kazi wakati sio kweli.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Kondoa na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa wakati wa kikao kazi chake na watumishi hao leo wilayani Kondoa chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Aidha, Mhe Ndejembi amewataka Maafisa Utumishi kuwa makini katika mchakato wa kuwapandisha madaraja watumishi wanaostahili kupanda na kuongeza kuwa Afisa Utumishi yeyote atakayebainika kusababisha mtumishi kutopata haki hiyo atachukuliwa hatua.

Mhe. Ndejembi amewasisitiza Watumishi wa Umma kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo katika Utumishi wa Umma ili kuboresha utendaji kazi utakaowezesha utoaji wa huduma bora kwa umma.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Mji Kondoa na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao leo wilayani Kondoa chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji Kondoa na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa leo Wilayani Kondoa, Mhe. Ndejembi amesema kuna baadhi ya Maafisa Utumishi hawatekelezi wajibu wao kikamilifu na kusababisha Ofisi ya Rais Utumishi kutupiwa lawama na Watumishi.

Amewaelekeza Wakurugenzi kuwasimamia Maafisa Utumishi wao ili watekeleze majukumu yao ipasavyo ikiwemo la kushughulikia fomu za madai ya malimbikizo ya watumishi hao ili yafanyiwe kazi kwa haraka kwa lengo la kupunguza malalamiko ya watumishi ambayo yanashusha ari ya kutekeleza majukumu yao kikamifu.

“Madai ya Watumishi yakichelewa kulipwa, mnasingizia fomu ziko UTUMISHI wakati sio kweli, mara nyingi fomu hizi zinakuwa ziko kwenu Wakurugenzi sababu Maafisa Utumishi wenu kujifanya miungu watu,’” Mhe. Ndejembi ameongeza.

Mhe. Ndejembi amesema madai ya Watumishi ni haki yao ya msingi kwani wanatumia jasho lao kulitumikia taifa, hivyo wanastahili kulipwa na si hisani.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Sezaria Makota akimshukuru Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi kwa kufanya ziara ya kikazi leo wilayani Kondoa yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma wilayani humo.

Akizungumzia changamoto ya upandishwaji madaraja kwa watumishi, Mhe. Ndejembi amewaelekeza Maafisa Utumishi nchini kuhakikisha wanatenda haki kwa wanaostahili kupandishwa madaraja kama Mhe. Rais Samia Suhuhu Hassan alivyoelekeza.

“Tujitume kwa bidii tusimuangushe Mhe. Rais ambaye ameonyesha nia thabiti ya kuwajali Watumishi wa Umma katika kulinda maslahi na haki zao za msingi,” Mhe. Ndejembi amesisitiza.
Mkurugenzi wa Halmshauri ya Mji Kondoa Bw. Msoleni Dakawa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya halmashauri yake kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na Watumishi wa Wilaya hiyo leo chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma wilayani humo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Kondoa Bw. Mustapha Semwaiko akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya halmashauri yake kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na Watumishi wa Wilaya hiyo leo chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma wilayani humo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Mhe. Sezaria Makota, amemshukuru Mhe. Ndejembi kwa kufika Wilayani humo na kuzungumza na Watumishi ambapo pia amesisitiza uwajibikaji kwa watumishi hao.

Mhe. Makota amesema hapendezwi kuwepo kwa madai ya malimbikizo ya mishahara na ya upandishwaji vyeo ambayo hayajafanyiwa kazi na Maafisa Utumishi katika Wilaya yake na kuongeza kuwa hatosita kuwachukulia hatua watakaoshindwa kutekeleza maelekezo.

Mhe. Mhe. Ndejembi amefanya ziara ya kikazi Wilayani Kondoa kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Mji Kondoa na Halmshauri ya Wilaya ya Kondoa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news