Tume ya Taifa ya Mipango imefanya mazungumzo na wadau wa maendeleo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa maendeleo na kuendeleza mahusiano ya kimkakati.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Katibu Mkuu wa Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dk.Tausi Kida amesema mazungumzo hayo yamelenga kujenga uelewa wa pamoja kuhusu vipaumbele vya maendeleo vya Tanzania vilivyoainishwa katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) na Dira ya Maendeleo ya 2050.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


























