Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, imetoa vifaa vya TEHAMA vyenye thamani ya jumla ya Sh. 769,390,000 kwa shule za msingi na sekondari 19 zilizopo katika mikoa tisa ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Vifaa hivyo vinajumuisha madarasa janja, mbao janja, vishikwambi na kompyuta, ambavyo vinatarajiwa kuwezesha ujifunzaji kwa wanafunzi, hususan katika masomo ya sayansi na teknolojia. Aidha, walimu watanufaika kwa kutumia mbinu bunifu za ufundishaji pamoja na mifumo ya kidijitali kufuatilia maendeleo ya wanafunzi kwa ufanisi zaidi.
Hafla ya ugawaji wa vifaa hivyo imefanyika Machi 30, 2026 jijini Dodoma, ambapo Naibu Waziri wa Elimu, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, alisisitiza dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita kuendeleza mageuzi makubwa katika sekta ya elimu kupitia matumizi ya teknolojia za kidijitali.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo



















